Biofueli

From Wikipedia, the free encyclopedia

Biofueli
Remove ads

Biofueli ni aina ya nishati inayozalishwa kutoka vyanzo vya kikaboni, kama mimea au viumbe hai vingine, badala ya kutegemea fueli za kisukuku ambayo ni mabaki ya viumbehai ya miaka mingi iliyopita kama mafuta ya petroli au makaa ya mawe. Biofueli hupatikana kama dutu mango, kiowevu au gesi.

Thumb
Biodiseli katika chupa.
Thumb
Katika nchi mbalimbali biofueli huuzwa kwa bei nafuu; hapa juu tangazo la biodiseli nchini Ujerumani.

Mara nyingi biofueli inatumika kama nishati mbadala ya kuendesha injini za magari na ndege, na hata kwa kuzalisha umeme au kuwasha moto nyumbani. Kwa kuzingatia upatikanaji wa vyanzo vyenye kaboni, biofueli inaonekana kama suluhisho linalopunguza utegemezi wetu kwa vyanzo vya nishati vinavyochangia mabadiliko ya tabianchi[1].

Kuna mbinu mbili hasa za kutengeneza biofueli:

Thumb
Basi litumialo biofueli inayotokana na soya.

Ethanoli hizi hutumiwa badala ya petroli na mafuta badala ya diseli katika injini ya mwako ndani.

Njia nyingine ni kutumia mbao au nyasi mbalimbali zilizokaushwa, na mara nyingi kukatwa na kupewa umbo la donge halafu kuchomwa kwa kutengeneza umeme.

Remove ads

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads