Chotara
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Chotara (kutoka Kihindi; pia: suriama kutoka Kiarabu na shombe) ni kiumbe hai ambacho kimetokana na makabila zaidi ya moja ya spishi yake. Kwa mfano, binadamu ambaye alizaliwa na baba Mzungu na mama Mwafrika anaitwa hivyo.[1]


Katika lugha mbalimbali kuna majina maalumu kwa aina za machotara: kwa mfano katika Kihispania kuna Mulato, zambo na mestizo; katika Kireno kuna mulato, caboclo, cafuzo, ainoko na mestiço.
Pengine sensa zinauliza asili ya wakazi, zikiacha nafasi ya kutaja asili zaidi ya moja.
Kundi la pekee ni Machotara wa Afrika Kusini waliotokana na mchanganyiko wa Wazungu, Waafrika na Wamalay na kutengwa chini ya sheria ya apartheid nchini Afrika Kusini.
Remove ads
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads