Rasi ya Chukchi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Rasi ya Chukchi
Remove ads

Rasi ya Chukchi (pia Rasi ya Chukotka; kwa Kirusi: Чуко́тский полуо́стров, Chukotskiy poluostrov au Чуко́тка Chukotka) ni rasi ya mashariki zaidi ya Asia. Upande wa mashariki inaishia kwenye Rasi Dezhnev karibu na kijiji cha Uelen.

Thumb
Mahali pa Rasi ya Chukchikatika Siberia ya Mashariki ya Mbali.
Thumb
Ramani inayoonyesha jinsi Rasi ya Chukchi iko karibu Alaska
Thumb
Rasi ya Chukchi. Ramani ya jeshi la Marekani 1947

Imepakana na Bahari ya Chukchi upande wa kaskazini, Bahari ya Bering upande wa kusini, na Mlango wa Bering upande wa mashariki. Rasi hii ni sehemu ya Okrug huru ya Chukotka ya Urusi [1]. Wakazi wake ni makabila ya watu asilia wa Siberia na walowezi wachache Warusi.

Tasnia kwenye rasi hiyo ni pamoja na madini (bati, risasi, zinki, dhahabu, na makaa ya mawe) uwindaji, ufugaji wa kulungu aktiki, na uvuvi.

Remove ads

Marejeo

Kusoma zaidi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads