Cluny

From Wikipedia, the free encyclopedia

Clunymap
Remove ads

Abasia ya Cluny (au Cluni, au Clugny), ilikuwa monasteri ya Wabenedikto, maarufu kwa kuongoza urekebisho wa utawa na wa Kanisa lote kuanzia karne ya 10.

Thumb
Abasia ya Cluny mwaka 2004.

Ilijengwa kwa mtindo wa Kiroma katika eneo la Burgundy, leo mkoa wa Saône-et-Loire, Ufaransa.

Mwanzilishi wake, William I wa Aquitania, mwaka 910 alimteua Berno wa Cluny awe abati wa kwanza, chini ya Papa Sergius III tu. Hivyo alionyesha njia ya kukwepa watawala wasiendelee kuingilia vyeo vya Kanisa kwa malengo yao ya kisiasa na ya kiuchumi badala ya yale yaliyokusudiwa ya kidini.

Monasteri nyingine nyingi zilifuata njia hiyo na kivyo kuinua hali ya kiroho ya utawa na wa Kanisa kwa jumla katika karne zilizofuata.

Mwaka 1790, wakati wa Mapinduzi ya Kifaransa, abasia iliporwa na kubomolewa kwa kiasi kikubwa.

Thumb
Coat of Arms of Cluny Abbey: "Gules two keys in saltire the wards upwards and outwards or overall a sword in pale argent".
Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads