Kidudu-kifuko

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kidudu-kifuko
Remove ads

Vidudu-kifuko ni vidudu wadogo sana wa faila Cycliophora wanaoishi kwenye sehemu za mdomo za kambamawe. Hadi sasa wamefunua kwenye spishi tatu za kambamawe: kambamawe wa Marekani (Homarus americanus), kambamawe wa Ulaya (Homarus gammarus) na kambamawe wa Unowe (Nephrops norvegicus)[1].

Thumb
Mchoro wa Symbion pandora ukionyesha mwili kama kifuko, mpare wa mdomo wenye minyiri, mkundu, sahani ya kujiambatisha na lava aliyeambatishwa kando.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...

Wapevu hutokea katika hatua mbili. Ile kubwa zaidi ni hatua ya kujilisha, ambayo ina urefu wa µm 350 na upana wa µm 120. Ina mwili unaofanana na kifuko na mdomo wenye mpare unaobeba minyiri na mkundu juu yake (tazama mchoro). Inashikamana na unywele wa kambamawe kwa njia ya sahani ya kunyonya. Katika hatua hii wanyama wanaweza kuzaa bila utungisho kwa kuchipua nakala za wenyewe[2].

Katika hatua ya ngono kuna jinsia mbili ambazo zote zina urefu wa µm 85 na upana wa µm 40. Dume hana mdomo, mkundu wala mfumo wa mmeng'enyo wa chakula, lakini ana korodani mbili. Jike ana mfumo wa mmeng'enyo wa chakula na yai moja. Baada ya utungisho, yai hukua na kuwa lava ambaye hufyonza mwili wa mama yake hadi ganda tu libaki. Kisha lava huogelea kwenda kutafuta mwenyeji mpya[2].

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads