Mdudu Mikia-miwili

From Wikipedia, the free encyclopedia

Mdudu Mikia-miwili
Remove ads

Wadudu mikia-miwili ni wadudu wadogo bila mabawa wa nusungeli Diplura (ngeli kufuatana na wataalamu wengi) katika nusufaila Hexapoda walio na mikia miwili ambayo siyo mikia kweli lakini serki (cerci) ndefu. Wana kiwiliwili kilichorefuka chenye urefu wa mm 2-5 (spishi kadhaa za jenasi Japyx zinaweza kufika mm 50). Hawana macho lakini wana vipapasio vyenye pingili 10 au zaidi kama shanga. Kiwiliwili hakina pigmenti isipokuwa serki nyeusi katika spishi kadhaa. Fumbatio inabeba vilengelenge vinavyofyonza unyevu kutoko mazingira (kama collophore kwa wadudu mkia-fyatuo). Wadudu hawa wanatokea katika udongo mnyevu, majani yaliyoanguka ardhini na mboji, na hula arithropodi wadogo sana, kuvu na maada ya viumbehai.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Remove ads

Picha

Makala hii kuhusu "Mdudu Mikia-miwili" inatumia neno (au maneno) ambalo si kawaida na matumizi yake ni jaribio la kutafsiri neno (au maneno) la asili Diplura kutoka lugha ya Kilatini. Neno (au maneno) la jaribio ni mdudu mikia-miwili.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao kwenye ukurasa wa majadiliano ya makala.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.

Remove ads
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads