Dorotheo wa Turo

From Wikipedia, the free encyclopedia

Dorotheo wa Turo
Remove ads

Dorotheo wa Turo (Antiokia ya Siria, leo nchini Uturuki, 255 hivi - Varna, Bulgaria, 362) alikuwa askofu wa mji huo wa Lebanoni [1].

Thumb
Mchoro mdogo kutoka Menologion ya Basili II.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 5 Juni[2][3].

Maisha

Dhuluma ya kaisari Diocletian ilimlazimisha kukimbia alipokuwa padri maarufu kwa elimu yake, lakini baadaye akarudi.

Alishiriki mtaguso wa kwanza wa Nisea mwaka 325, lakini alifukuzwa na kaisari Juliani Mwasi akakae Odyssopolis (Varna, leo nchini Bulgaria) kwenye Bahari Nyeusi. Huko alifia dini yake akiwa na umri wa miaka 107[4].

Maandishi

Anasemekana kuwa mwandishi wa kitabu "Matendo ya Wanafunzi Sabini" waliotumwa na Yesu kadiri ya Injili ya Luka 10:1.

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads