Epafra

From Wikipedia, the free encyclopedia

Epafra
Remove ads

Epafra (kwa Kigiriki Ἐπαφράς, Epafras; alifariki Kolosai, 80) alikuwa mwanafunzi na msaidizi wa Mtume Paulo katika uinjilishaji wa mji wa Efeso na mkoa wa Asia.

Thumb
Sanamu ya Mt. Epafra.

Inaonekana alikuwa mwenyeji wa Kolosai na alitumwa kueneza Ukristo huko (Kol 1:7; 4;12-13) pamoja na Laodikea na Yerapoli.

Baada ya muda, yalijitokeza huko matatizo ya kiimani yaliyomfanya Paulo aandike barua maarufu kama Waraka kwa Wakolosai.

Paulo anamtaja pia kama mfungwa mwenzake (Waraka kwa Filemoni 1:23).

Kwa jinsi alivyomsifu, kama mshiriki mpenzi wa kazi yake na mtumishi mwaminifu wa Kristo, tangu kale anaheshimiwa na madhehebu mengi kama mtakatifu[1].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 19 Julai[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads