Euphrase Kezilahabi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Euphrase Kezilahabi (Namagondo, Ukerewe, 13 Aprili 1944 - 9 Januari 2020, Dar es Salaam) alikuwa mwandishi mashuhuri kutoka nchini Tanzania. Lugha yake ya kwanza ilikuwa Kikerewe lakini aliandika hasa kwa Kiswahili ambacho amekipanua kwa kutumia mitindo ya lugha yake ya asili.

Maisha

Euphrase Kezilahabi alizaliwa 13 Aprili 1944 huko Namagondo kisiwani Ukerewe kilichopo ndani ya Ziwa Viktoria. Babake Vincent Tilibuzya alikuwa msimamizi wa kijiji na Euphrase alikuwa na ndugu 10 yaani wavulana 5 na wasichana 5. Alisoma shule ya msingi ya Nakasayenge halafu tangu 1957 Seminari ya kikatoliki ya Nyegezi aliyomaliza mwaka 1966. [1]

Mwaka 1967 alijiandiskisha kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akasoma ualimu na fasihi hadi digrii ya B.A. katika mwaka 1970. Mwaka uleule 1970 akawa mwalimu wa shule ya sekondari Mzumbe (Morogoro) halafu kwenye shule ya sekondari ya Mkwawa (Iringa).

Mwaka 1971 alirudi chuoni Dar es Salaam akawa mhadhiri msaidizi wa chuo alipoandika pia tasinifu ya M.A. kuhusu riwaya za Shaaban Robert, tangu 1974 mhadhiri kamili na 1978 mhadhiri mwandamizi. Akaendelea na masomo ya Ph.D. huko Marekani kwenye Chuo Kikuu cha Wisconsin Madison alipotoa tasinifu yake mwaka 1985 kuhusu "African Philosophy and the Problem of Literary Interpretation". Mwaka 2012 alikuwa profesa wa lugha za Kiafrika kwenye Chuo Kikuu cha Botswana.

Mwaka 2020 aliaga dunia akiwa jijini Dar es Salaam baada ya kuugua kwa muda mrefu[2].

Remove ads

Maandiko

Baadhi ya maandiko yake ni:

Riwaya:

Mashairi:

  • Kichomi (1974)
  • Karibu Ndani (1988)
  • Dhifa (hakijatolewa bado)

Tamthiliya:

Marejeo

Viungo vya Nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads