Gentile wa Fabriano

From Wikipedia, the free encyclopedia

Gentile wa Fabriano
Remove ads

Gentile wa Fabriano (1370 hivi – 1427) alikuwa mchoraji wa Italia aliyefanya kazi hasa katika mkoa wa Toscana.

Thumb
Ibada ya Mamajusi (1423)
Thumb
Bikira Maria katika Ibada ya Mamajusi (1423).

Michoro yake maarufu zaidi inawahusu Yesu na Bikira Maria, nayo ni Ibada ya Mamajusi (1423) na Kukimbilia Misri.

Maisha

Gentile alizaliwa Fabriano, katika dola la Papa, (leo mkoa wa Marche).

Kabla ya mwaka 1380 mama yake alifariki, na hapo baba yake, Niccolò di Giovanni Massi, alijiunga na monasteri, alipofariki mwaka 1385. Hakuna habari zaidi kuhusu malezi yake.

Mwaka 1405 hivi, Gentile alikuwa akifanya kazi huko Venice, halafu akachora huko Fabriano, Foligno, Brescia, halafu tena Fabriano.

Thumb
Bikira Kutiwa Taji

Tarehe 6 Agosti 1420 alikuwa Florence, halafu Siena, Orvieto na hatimaye mwaka 1427 alifika Roma, alipopata agizo la Papa Martin V, lakini hakumaliza kulitekeleza kwa sababu alifariki kabla ya tarehe 14 Oktoba.

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads