Georgia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Georgia ni nchi iliyoko kati ya Ulaya ya Mashariki na Asia ya Magharibi. Ni sehemu ya eneo la Kaukazi, ikipakana na Bahari Nyeusi upande wa magharibi, Urusi upande wa kaskazini na kaskazini-mashariki, Uturuki upande wa kusini-magharibi, Armenia upande wa kusini, na Azerbaijan upande wa kusini-mashariki.
Kwa matumizi mengine ya jina hili, tazama Georgia (maana).
Georgia inachukua eneo la kilomita za mraba 69,700 (maili za mraba 26,900). Ina idadi ya watu milioni 3.7, ambapo zaidi ya theluthi moja wanaishi katika mji mkuu na mji mkubwa zaidi, Tbilisi. Wenyeji wa Georgia, ambao ni asili ya eneo hilo, wanaunda sehemu kubwa ya idadi ya watu wa nchi hiyo na ndio taifa kuu.
Remove ads
Jiografia
Georgia ni nchi ya milima inayofikia kimo cha mita 5,068. Kati ya safu mbili za milima kuna tambarare ya Kolkhis.
Upande wa magharibi unafaidika zaidi na Bahari Nyeusi, hivyo una hali ya hewa safi na mvua nyingi inayofaa kwa kilimo hasa cha mizabibu.
Historia
Georgia ilikuwa sehemu ya Umoja wa Kisovyeti lakini imekuwa nchi huru tangu 1991.
Maeneo ya Abkhazia na Ossetia ya Kusini yamedai uhuru pia na kwa sasa hayapo chini ya serikali kuu, lakini hayatambuliki kimataifa.
Utamaduni
Wakazi walio wengi (71%) huzungumza lugha ya Kigeorgia lakini kuna vikundi vya wazungumzaji wa Kirusi (9%), Kiarmenia (7%), Kiazeri (6%) na lugha nyingine.
Wageorgia wengi ni Wakristo wanaofuata Kanisa la Kiorthodoksi la Georgia (83.9%). Kuna pia wafuasi wa Kanisa la Kitume la Armenia (3.9%) na Wakatoliki (0.8%). Waislamu ni 9.9%, wakati Wayahudi wanazidi kuhama.
Watu maarufu
Mgeorgia anayejulikana zaidi duniani alikuwa Josef Stalin, mtawala wa Urusi wakati wa Ukomunisti.
Tazama pia
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads