Gilbati wa Neuffonts

From Wikipedia, the free encyclopedia

Gilbati wa Neuffonts
Remove ads

Gilbati of Neuffonts, O. Praem. (Auvergne, leo nchini Ufaransa, mwishoni mwa karne ya 11 - Saint-Didier-la-Forêt, Ufaransa, 6 Juni 1152) alikuwa mkabaila aliyeishi kama mkaapweke kwa miaka michache kabla hajajiunga na shirika la Wakanoni wa Premontree, na kufanywa abati.

Thumb
Sanamu yake huko Bad Schussenried, Ujerumani.

Kabla ya kutawa alikuwa na mke na binti mmoja akashiriki katika vita vya Msalaba (1146). Baada ya kukubaliana na mwenzake wa ndoa, alianzisha monasteri ya kike huko Aubeterre iliyoongozwa kwanza na mke wake, halafu na binti yao. Alianzisha pia hospitali kwa ajili ya wakoma na monasteri ya kiume huko Neufforts[1].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu. Papa Benedikto XIII alithibitisha heshima hiyo tarehe 22 Januari 1728.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 6 Juni[2]

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads