Goeriki

From Wikipedia, the free encyclopedia

Goeriki
Remove ads

Goeriki (pia: Goheric, Goderic, Goëry, Goeric, Goericus, Goéry, Abbo, Appo, Abdo, Albo; Albi, leo nchini Ufaransa[1], 565/575 [2] - 643 hivi) alikuwa mwanajeshi mwenye cheo kikubwa[3] chini ya Dagobati I, mfalme wa Austrasia.

Thumb
Mt. Goeriki katika mavazi ya ibada ya kiaskofu.

Baba wa mabinti wawili, ambaye mmojawao (Prisia) anaheshimiwa kama mtakatifu bikira, mwaka 627 alichaguliwa kuwa askofu wa Metz[4] baada ya Arnulfo, ambaye labda alikuwa jamaa yake na alimpa upadirisho, kwenda kwa siri kuishi kama mkaapweke karibu na monasteri ya Hamend iliyoanzishwa na rafiki yake Amato[5].

Arnulfo alipofariki, Goeriki alihamisha kwa heshima zote masalia yake mjini Metz [6].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 19 Septemba[7].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads