Hagar
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Hagar (kwa Kiebrania: הָגָר, *Hāgār*, jina lenye asili isiyojulikana[1]; kwa Kiarabu: هَاجَر, *Hājar*; kwa Kigiriki: Ἁγάρ, *Hagár*; kwa Kilatini: *Agar*) ni mhusika wa Biblia aliyekuwa mtumwa wa Misri na mjakazi wa Sara (wakati huo aliitwa Sarai).[2]
Sara alimpa Hagar kwa mume wake Abramu (baadaye Abrahamu) kuwa suria wake, ili aweze kumzalia mtoto kwa sababu Sarai alikuwa tasa kwa muda mrefu. [3]
Baada ya Hagar kupata mimba, mvutano ulizuka kati yake na Sarai. Kitabu cha Mwanzo kinasema kuwa Hagar alimdharau Sarai, jambo lililomfanya Sarai amtese Hagar hadi akaamua kukimbia. [4]
Mtoto wa Hagar aliitwa Ishmaeli, ambaye alikua baba wa Waishmaeli. Katika mapokeo ya Kiarabu, Ishmaeli huhesabiwa kuwa babu wa Waarabu na Hagar huhesabiwa kuwa mama wa taifa hilo. [5] [6] [7] [8]
Hagar hatajwi kwa jina katika Kurani, lakini anaheshimiwa katika Uislamu kama mke wa pili wa Abrahamu na mama wa Ishmaeli, ambaye Mtume Muhammad anahesabiwa kama mzao wake.
Remove ads
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads