Hedwiga wa Polandi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Hedwiga (kwa Kijerumani Hedwig; kwa Kipolandi Jadwiga, linatamkwa jadˈviɡa; Budapest, Hungaria, 1373/1374 - Krakov, Polandi, 17 Julai 1399) alikuwa malkia wa Polandi na Lituanya.


Kuanzia mwaka 1384 hadi kifo chake alitawala nchi ya Polandi akiitwa 'mfalme' badala ya 'malkia', ili kusisitiza kwamba hakuwa tu mke wa mtawala halisi[1].
Alizaliwa katika ukoo wa Wakapeti wa Anjou, binti wa mwisho wa mfalme Luis I wa Hungaria na Elizabeti wa Bosnia.[2].
Kwa kuolewa na Ladislaus wa Lituania, alimfanya abatizwe akaeneza Ukristo katika nchi hiyo ya Kipagani [3].
Tangu zamani anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu na msimamizi wa kila malkia. Papa Yohane Paulo II ndiye aliyemtangaza rasmi mwenye heri tarehe 8 Agosti 1986 na mtakatifu tarehe 8 Juni 1997.
Remove ads
Picha
- Uanzishwaji mpya wa Kraków Academy uliofanywa na Hedwiga.
- Kikombe cha Hedwiga kutoka Wawel Cathedral.
- Mhuri wa Hedwiga wa Polandi
- Maziara ya Hedwiga na Jagiełło (Jogaila) huko Kraków, Planty Park.
- Hedwiga alivyochorwa na Antoni Piotrowski hapo baadaye.
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads