Isidori wa Pelusio

From Wikipedia, the free encyclopedia

Isidori wa Pelusio
Remove ads

Isidori wa Pelusio (kwa Kigiriki: Ἰσίδωρος ὁ Πηλουσιώτης; alifariki 450 hivi) alikuwa mmonaki padri wa Misri.

Thumb
Isidori wa Pelusium.

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi wa Mashariki na Wakatoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 4 Februari[1].

Maisha

Mtoto pekee wa familia maarufu wa Aleksandria[2], akiwa ameshajipatia ujuzi mwingi, alitawa kwenye mlima karibu na mji wa Pelusium, kwa kufuata nyayo za Yohane Mbatizaji na Mababu wa jangwani [3].

Pia alijitosa kuhubiri kwa mfano wa Yohane Krisostomo akamtetea dhidi ya dhuluma kutoka kwa patriarki Theofilo wa Aleksandria, ndugu yake, na kwa malkia Eudosia.

Maandishi

Anajulikana kwa barua 2,000 hivi alizowaandikia patriarki Sirili wa Aleksandria, kaisari Theodosius II na wengineo wengi.[4] Baadhi yake ni muhimu kwa ufafanuzi wa Biblia.[5]

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads