Ja Rule
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Jeffrey Atkins (amezaliwa tar. 29 Februari, 1976),[1] anafahamika kwa jina lake la kisanii Ja Rule, ni rapa kutoka nchini Marekani, mwimbaji, na vilevile mwigizaji kutoka mjini Queens, New York.
Remove ads
Alizaliwa mjini Hollis, Queens, alianza kutamba kunako mwaka wa 1999 akiwa na albamu ya Venni Vetti Vecci na kibao chake kikali cha "Holla Holla". Kuanzia 1999 hadi 2005, Ja Rule amekuwa na vibao kadhaa vilivyoingia kwenye 20 bora ya chati za Billboard Hot 100, ikiwa ni pamoja na "Between Me and You" akishirikiana na Christina Milian, "I'm Real (Murder Remix)" na Ain't It Funny akiwa na Jennifer Lopez, ambazo zote zilitingisha katika chati za US Billboard Hot 100, kibao namba 1 kilichobahatika kuchaguliwa katika Tuzo za Grammy, "Always on Time" akiwa na Ashanti, "Mesmerize" nacho pia alikuwa na Ashanti, na "Wonderful" akiwa na R. Kelly na Ashanti.
Wakati wa miaka ya 2000, Ja Rule aliingia mkataba na The Inc. Records, ambayo awali ilikuwa ikitambulika kama Murder Inc. na ilikuwa ikiongozwa na Irv Gotti. Kutokana na vibao vyake na washirika wake, Ja Rule amepokea chaguzi nne za Grammy, na albamu zake sita zimeiingia katika kumi bora, mbili katika hizo ni Rule 3:36 (2000) na Pain Is Love (2001), imegonga vyema katika chati za US Billboard 200. Pia anafahamika sana katika jamii kwa kuwa na mgogoro na baadhi ya marapa wengine kama vile (hasa 50 Cent na Eminem).
Remove ads
Maisha ya awali
Kazi ya muziki
Diskografia
- Albamu za Studio
- 1999: Venni Vetti Vecci
- 2000: Rule 3:36
- 2001: Pain Is Love
- 2002: The Last Temptation
- 2003: Blood in My Eye
- Albamu zingine
- 2004: R.U.L.E.
- 2012: Pain Is Love 2[2]
- Albamu huru
- 2009: The Mirror
- Albamu za kompilesheni
- 2005: Exodus
- 2012: Icon
Marejeo
Viungo vya Nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads