Jabari
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Jabari ni kundinyota linalojulikana pia kwa jina lake la kimagharibi la Orion. Ni moja ya makundinyota yanayotambuliwa na Umoja wa Kimataifa wa Astronomia [1]


Nyota za Jabari huwa hazipo pamoja kihalisi lakini zinaonekana tu vile kutoka duniani. Kwa uhalisia kuna umbali mkubwa kati yake, kama ziko mbali au jirani nasi. Kwa hiyo kundinyota "Jabari" linaonyesha eneo la angani jinsi tunavyoliona kutoka duniani.
Remove ads
Jina
Jina la Kiswahili ni Jabari na linatokana na Kiarabu الجبار al-jabbaar ambalo linamaanisha "jitu". Jina hili lilipokewa na Waarabu kutoka kwa Waaramu waliosema gabbara "jitu"[2]. Wote walimaanisha hapa tabia ya mwindaji mkuu na nusu-mungu katika mitholojia ya Kigiriki aliyeitwa Ὠρίων orion na hivyo alitajwa katika kitabu cha Almagesti cha Klaudio Ptolemaio.
Nyota
Jabari ni kati ya makundinyota yanayoonekana vyema kwenye angakusi na pia angakaskazi ya Dunia. Nyota saba angavu sana zinakumbukwa kirahisi na watazamaji wa anga.
Nyota nne za Rijili ya Jabari (Rigel), Ibuti la Jauza (Betelgeuse), Bellatrix and Saiph zinafanya pembenne, na katikati kuna safu ya nyota tatu za karibu zinazoitwa "ukanda" ambazo ni Alnitak, Alnilam na Mintaka (ζ, ε na δ Orionis). Chini ya nyota za ukanda kuna nyota angavu inayotambuliwa kwa darubini ndogo kuwa nebula angavu, hii ni Nebula ya Jabari (Orion nebula).
Remove ads
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya Nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads