Joji Preca

From Wikipedia, the free encyclopedia

Joji Preca
Remove ads

Joji Preca (kwa Kimalta: Ġorġ; La Valletta, Malta, 12 Februari 1880[1] - Santos Vendroob, Malta, 26 Julai 1962) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki nchini Malta aliyeshughulikia hasa malezi na katekesi ya vijana[2]. Kwa ajili hiyo alianzisha Shirika la Mafundisho ya Kikristo ili kuonyesha Neno la Mungu linavyofanya kazi ndani ya taifa lake.

Thumb
Sanamu ya Mt. Joji.

Ndiye aliyebuni mafumbo ya mwanga ya Rozari[3].

Papa Yohane Paulo II alimtangaza kuwa mwenye heri tarehe 9 Mei 2001[4], na Papa Benedikto XVI alimtangaza mtakatifu tarehe 3 Juni 2007, wa kwanza kutoka nchi hiyo ya Ulaya visiwani[5].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyoaga dunia[6].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads