Rozari

From Wikipedia, the free encyclopedia

Rozari
Remove ads

Rozari (kutoka Kilatini rosarium, yaani "taji la mawaridi"),[1] ni ushanga uliotengenezwa kwanza na Wakatoliki wa Karne za Kati ili kusali kwa kukariri Salamu Maria kadhaa pamoja na kutafakari mafumbo ya imani.

Thumb
Rozari pamoja na Biblia na Msulubiwa.

Historia

Thumb
Mafumbo 15 ya msingi ya Rozari na Bikira Maria wa Rozari.

Shanga zilitumika kama pambo tangu kale: barani Afrika zimepatikana za miaka 10,000 KK.

Lini na wapi zilianza kutumika kwa ajili ya sala haijulikani, lakini kuna sanamu ya karne ya 3 KK inayomuonyesha Mhindu akiwa na ushanga wa sala.

Lengo ni kutunza hesabu ya kauli ambazo zinakaririwa kwa kupitisha vidole viwili juu ya punje zilizounganishwa katika kamba au uzi.

Wakristo wa karne ya 15 waliotamani kusali kama watawa Zaburi 150, lakini hawakujua Kilatini au kusoma kabisa, walijifunza kwa urahisi kukariri Salamu Maria 150 huku wakitafakari mafumbo ya maisha ya Yesu, kama alivyowahi kufanya Dominiko wa Prussia (1382-1460), mmonaki Mkartusi.[2]

Lakini shirika lililojihusisha zaidi na Rozari ni lile la Wadominiko.[3][3][4][5][6]

Mwaka 1569, Papa Pius V aliyekuwa wa shirika hilo, alipitisha sala hiyo kwa Kanisa lote, akapanga mgawanyo wa mafumbo 15 na kukabidhi uenezi wake kwa Wadominiko wenzake.

Mafumbo hayo yaligawiwa katika makundi matatu: 5 ya furaha (utoto wa Yesu), 5 ya uchungu (mateso ya Yesu) na 5 ya utukufu (ufufuko wa Yesu na yatokanayo). Kila fumbo lina Salamu Maria 10, zikitanguliwa na Baba Yetu na kumalizika kwa Atukuzwe.

Mwaka 2002 Papa Yohane Paulo II alipendekeza kuongeza mafumbo 5 ya mwanga ili kuziba pengo kuhusu miaka ya utume wa Yesu.[7]

Mbali na hao, Mapapa wote walihimiza sala hiyo kama njia rahisi kwa wote ya kukumbuka na kuheshimu kazi ya wokovu iliyofanywa na Yesu Kristo.[8]

Sala hiyo imeenea katika baadhi ya madhehebu mengine ya Ukristo, hasa Anglikana.

Remove ads

Mafumbo ya Rozari

Mafumbo ya furaha
  1. Bikira Maria Kupashwa habari. Tunda: Unyenyekevu
  2. Bikira Maria kumtembelea Elizabeti. Tunda: Upendo kwa jirani
  3. Yesu kuzaliwa. Tunda: Ufukara
  4. Yesu kutolewa hekaluni. Tunda: Utiifu
  5. Yesu kupatikana siku ya tatu hekaluni. Tunda: Hekima
Mafumbo ya mwanga
  1. Ubatizo wa Yesu. Tunda: Uwazi kwa Roho Mtakatifu
  2. Arusi ya Kana. Tunda: Kwa Yesu kumpitia Maria
  3. Yesu akitangaza Ufalme wa Mungu. Tunda: Kumtegemea Mungu
  4. Yesu kugeuka sura. Tunda: Hamu ya utakatifu
  5. Yesu kuweka Ekaristi. Tunda: Ibada
Mafumbo ya uchungu
  1. Kihoro cha Yesu bustanini. Tunda: Chuki kwa dhambi
  2. Yesu kupigwa mijeledi. Tunda: Kiasi
  3. Yesu kutiwa taji la miba. Tunda: Ushujaa
  4. Yesu kubeba msalaba. Tunda: Uvumilivu
  5. Yesu msalabani. Tunda: Wokovu, Msamaha
Mafumbo ya utukufu
  1. Ufufuko wa Yesu. Tunda: Imani
  2. Yesu Kupaa mbinguni. Tunda: Tumaini
  3. Pentekoste. Tunda: Upendo kwa Mungu, utume
  4. Maria Kupalizwa mbinguni. Tunda: Neema ya kufa vema
  5. Maria kutukuzwa mbinguni. Tunda: Udumifu
Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads