Kasio wa Narni

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Kasio wa Narni (alifariki Narni, Italia ya Kati[1], 29 Juni 558 BK) anakumbukwa kama askofu wa mji huo kuanzia mwaka 536 hadi kifo chake[1].

Aliwahi kuoa Fausta lakini baadaye alimuacha aishi kitawa[2]. Alikuwa maarufu kwa upendo wake kwa maskini hata akasifiwa na Papa Gregori I, anayesimulia alivyomtolea Mungu kila siku sadaka ya upatanisho kwa kumwaga machozi mengi na alivyokuwa anatoa kwa wahitaji kila alichokuwanacho. Hatimaye, siku ya kuadhimisha sherehe ya Mitume Petro na Paulo, ambayo alizoea kwenda kila mwaka huko Roma, kisha kuadhimisha Misa na kuwapatia wote Mwili wa Kristo katika mji wake, alirudi kwa Bwana.[3].[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[4]

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads