Kiribati

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kiribati
Remove ads


Kiribati rasmi kama Jamhuri ya Kiribati, ni nchi ya kisiwa iliyoko katika Pasifiki ya kati, ikivuka ikweta. Inaundwa na visiwa 33 vya atoli na miamba, vilivyotawanyika katika eneo kubwa la bahari, na majirani yake wa karibu ni Tuvalu kusini, Nauru magharibi, na Visiwa vya Marshall kaskazini-magharibi. Kiribati ina wakazi 120,000 na kwa hiyo iko kati ya nchi ndogo zaidi kwa idadi ya watu.Mji mkubwa zaidi na mji mkuu wa Kiribati ni Tarawa kusini, uliopo kwenye atoli ya Tarawa na hutumika kama kitovu cha kisiasa na kiuchumi cha nchi hiyo.

Thumb
Ramani ya Kiribati
Ukweli wa haraka
Remove ads

Jiografia

Kiribati ina eneo pana sana; umbali kati ya kisiwa cha magharibi kabisa cha Banaba hadi kisiwa cha mashariki kabisa cha Millenium ni kilomita 4,835; umbali wa kaskazini-kusini ni km. 1,973.

Eneo hili liko katikati ya Hawaii na Australia.

Karibu visiwa vyote havipiti kimo cha mita 2 juu ya UB. Kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa duniani na kupanda kwa uwiano wa bahari wataalamu wamekadiria ya kwamba nchi itazama kabisa katika hii karne ya 21.

Remove ads

Lugha na dini

Kuna lugha mbili tu nchini Kiribati, zote mbili zikiwa lugha rasmi, yaani Kiingereza na hasa Kikiribati.

Upande wa dini, linaongoza Kanisa Katoliki (56%), likifuatwa na madhehebu mbalimbali ya Uprotestanti.

Tazama pia


Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads