Kunguni-mgunda

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kunguni-mgunda
Remove ads

Kunguni-mgunda ni wadudu wadogo hadi wakubwa kiasi wa oda ya chini Pentatomomorpha katika oda Hemiptera ya nusungeli Pterygota (wenye mabawa) ambao wana mabawa ya mbele yaliyo nusu magumu na nusu kama kiwambo. Takriban wadudu hao wote hufyonza utomvu wa mimea, matunda au mbegu, lakini spishi nyingine hula kuvu na nyoga au wadudu wadogo. Spishi fulani huitwa visulisuli pia.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...

Mifano ya wadudu hao ni kunguni-ngao (familia Pentatomidae), kunguni-bapa (familia Aradidae), kunguni-mbegu (familia Lygaeidae na Rhyparochromidae) n.k.

Remove ads

Maelezo

Miundo na ukubwa ya kunguni-mgunda yanatofautana sana. Lakini, sifa zao ni sehemu za mdomo zinazotoboa ili kufyonza vioevu na mabawa ya mbele yaliyo nusu magumu na nusu kama viwambo. Takriban spishi zote hufyonza utomvu kutoka mashina, matunda na mbegu. Spishi chache kiasi hujilisha kwa wadudu wadogo au kuvu.

Kama wadudu mabawa-nusu wote lava za Pentatomomorpha zinafanana na wapevu. Kwa kawaida kuna hatua tano na ile ya mwisho inaambua kuwa mpevu mara moja bila kupita kwa hatua ya bundo. Mayai hutagwa juu ya mimea mara nyingi. Spishi za Aradoidea zinataga chini ya gome la miti au chini ya takataka ya majani. Spishi fulani hubeba mayai mgongoni.

Remove ads

Spishi kadhaa za Afrika ya Mashariki

  • Anoplocnemis curvipes (Coreidae)
  • Antestiopsis thunbergii (Pentatomidae)
  • Clavigralla tomentosicollis (Coreidae)
  • Dysdercus cardinalis (Pyrrhocoridae)
  • Dysdercys fasciatus (Pyrrhocoridae)
  • Dyscerdus nigrofasciatus (Pyrrhocoridae)
  • Geocoris ruficeps (Lygaeidae)
  • Oxycarenus hyalinipennis (Lygaeidae)
  • Probergrothius angolensis (Pyrrhocoridae)
  • Pseudotheraptus wayi (Coreidae)
  • Usambaraia ampliata (Aradidae)

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads