Lugha za Kihindi-Kiirani

From Wikipedia, the free encyclopedia

Lugha za Kihindi-Kiirani
Remove ads

Lugha za Kihindi-Kiirani ni kundi kubwa zaidi katika familia ya lugha za Kihindi-Kiulaya. Zinajumuisha lugha za Kihindi-Kiarya na lugha za Kiirani (Irani). Zinazungumzwa zaidi kwenye Bara Hindi na Nyanda za Juu za Iran. Hapo zamani zilitumiwa pia katika Asia ya Kati, mashariki mwa Bahari ya Kaspi .

Thumb
Lugha za Kihindi-Kiulaya; buluu: maeneo ya lugha za Kihindi-Kiirani

Lugha za Kihindi-Kiarya

Kuna karibu lugha 221 za Kihindi-Kiarya (Kiing. Indic), zenye jumla ya wasemaji zaidi ya milioni 800.

Remove ads

Lugha za Kiirani (Kiajemi)

Kuna karibu lugha 86 za Kiirani, zenye wasemaji kati ya milioni 150 hadi 200.

Kinuristani, Kibangani, na Kibadeshi

Wasomi wengine huchukulia lugha za Kinuristani na Kibangani kama sehemu ya kikundi kidogo cha Kihindi-Kiarya, lakini wengine wanazichukulia kama vikundi viwili tofauti vya Kihindi-Kiirani. Lugha ya Kibadeshi pia ni lugha ya Kihindi-Kiirani isiyopangwa bado kimakundi.

Vyanzo

  • Cardona, George. Indo-Iranian languages. Encyclopædia Britannica. Iliwekwa mnamo 27 Agosti 2018.{{cite encyclopedia}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  • Indo-Iranian. Ethnologue. Iliwekwa mnamo 27 Agosti 2018.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: others (link)
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads