Malaika walinzi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Malaika walinzi
Remove ads

Malaika walinzi ni malaika wanaosadikiwa kuwa, mbali ya kutazama utukufu wa Mwenyezi Mungu, wametumwa naye kuongoza na kulinda binadamu mmojammoja au katika makundi madogo na makubwa katika safari ya maisha kwa uwepo wao ambao hauonekani lakini unawajibika [1][2]

Thumb
Picha takatifu ya malaika mlinzi kutoka Urusi.
Thumb
Malaika mlinzi alivyochorwa na Pietro da Cortona, 1656.

Katika kalenda ya liturujia ya Kanisa la Kilatini, kumbukumbu yao inafanyika kila mwaka tarehe 2 Oktoba[3]. Kwa Waorthodoksi ni tarehe 11 Januari.

Remove ads

Historia ya imani hiyo

Imani hiyo ni ya zamani sana, ilijitokeza tayari katika Ugiriki wa Kale na katika Agano la Kale[4] na katika Agano Jipya[5], lakini ilistawishwa zaidi na Ukristo katika karne ya 5[6].

Imani ya namna hiyo katika Uislamu inapatikana katika Mu'aqqibat[7]

Sala kwa malaika mlinzi

Kwa Kilatini malaika mlinzi anaweza kuombwa hivi:

Angele Dei,
qui custos es mei,
me, tibi commissum pietate superna,
illumina, custodi,
rege et guberna.
Amen.[8]

Tafsiri yake ni:

Ee malaika wa Mungu,
uliye mlinzi wangu,
niliyewekwa kwako na huruma yake Mungu,
uniangaze, unilinde,
uniongoze, unitunze.
Amina.

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads