Matilda wa Ringelheim

From Wikipedia, the free encyclopedia

Matilda wa Ringelheim
Remove ads

Matilda wa Ringelheim (kwa Kijerumani Mathilde von Ringelheim; 894/89714 Machi 968) alikuwa malkia mdogo wa Saxony kuanzia mwaka 912 na malkia wa Ujerumani mzima kuanzia mwaka 919 kutokana na ndoa yake na Henry I, mfalme wa kwanza wa nasaba ya Otto.

Thumb
Mfalme Henry I na Matilda, kutoka Chronica sancti Pantaleonis, karne ya 12.

Mke mwaminifu kabisa, alikuwa na unyenyekevu na subira sana; pia alijitahidi kusaidia watu fukara na kujenga hospitali na monasteri [1].

Baada ya kufiwa mumewe mwaka 936, alianzisha abasia ya Quedlinburg kwa heshima yake. Matilda aliishi hadi kuona Dola la Roma la Magharibi kuanzishwa tena na mwanae wa kwanza, Otto I aliyetiwa taji mwaka 962.

Baada ya hapo alikwenda kutawa katika abasia hiyo ambapo ndipo alipofariki.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa katika tarehe ya kifo chake, 14 Machi[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads