Gambia (mto)

From Wikipedia, the free encyclopedia

Gambia (mto)
Remove ads

Gambia ni mto unaoanza katika milima ya Futa Djalon huko Guinea. Unafuata njia ya kunyoka hadi Atlantiki. Mdomo wake ni pana sana.

Ukweli wa haraka Mto Gambia ...

Baada ya kutoka katika Futa Djallon mto unaelekea kaskazini-magharibi kupitia mkoa wa Tambakunda katika Senegal halafu mbuga wa wanyama wa Niokolo Koba. Hapa inapokea tawimiti ya Nieri Ko and Kuluntu na kuingia katika nchi ya Gambia karibu na mji wa Fatoto.

Thumb
Mto Gambia ukipitia mbuga wa Niokolo-Koba nchini Senegal

Kuanzia hapa mto unaelekea magharibi tu isipokuwa kwa njia ya kunyokanyoka. Takriban km 100 kabla ya kufika mdomo unaanza kupanuka ukiwa na upana wa km 10 mdomoni penyewe.

Mto una visiwa mbalimbali ndani yake, vikubwa zaidi ni kisiwa cha Tembo na kisiwa cha MacCarthy. Kisiwa cha James Island mdomoni kabisa kilikuwa kituo muhimu cha biashara ya watumwa na kimeandikishwa katika orodha ya UNESCO ya Urithi wa Dunia.

Kutokana na upana na wingi wa maji Gambia inafaa kama njia ya maji; meli za baharini zinaingia ndani takriban km 280.

Miji mikubwa zaidi mtoni ni Basse Santa Su, Janjanbureh na Banjul.

Remove ads

Tazama pia

Viungo vya nje

en: The Gambia Basin Ilihifadhiwa 10 Mei 2006 kwenye Wayback Machine.

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads