Fungo-miti wa Afrika

From Wikipedia, the free encyclopedia

Fungo-miti wa Afrika
Remove ads

Fungo-miti (wa Afrika) (jina la kisayansi: Nandinia binotata) ni mnyama mbuai mdogo, spishi pekee ya jenasi yake na ya familia yake Nandiniidae[1]. Hii ni spishi ya misitu mizito ya Afrika ambapo huishi mitini. Mnyama huyu ni mpweke na hukiakia usiku.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi ...

Ana mwili ufananao na ule wa paka mdogo wenye miguu mifupi, masikio madogo na mkia wa urefu uleule wa mwili. Wanyama wazima huwa na uzito wa kg 1.7 hadi 2.1.

Hula vitu vyingi kama wagugunaji, wadudu, mayai, mizoga, matunda, ndege na popo-matunda. Fungo-miti ni mnyama ambaye hula sana bila kujali kesho. Hulka ya kula kwake imeleta msemo "Unakula sana kama Fungo" Ni nadra kuona kinyesi chake maana huwa na sehemu moja ya kuendea choo kama vile paka, pia njia anayoitumia ni moja tu.

Ijapo fungo-miti anafanana na spishi za fungo za familia Viverridae, inaonekana ni tofauti kinasaba na aliachana na fungo kabla ya paka. Kwa hiyo amepewa jenasi na familia yake binafsi, lakini kuna wataalamu ambao hawakubali.

Remove ads

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads