Popo

From Wikipedia, the free encyclopedia

Popo
Remove ads

Popo ni mamalia kama panya wenye mabawa.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...

Spishi zake nyingi sana hula wadudu: hizi zimo katika nusuoda Yangochiroptera.

Spishi kubwa za nusuoda hii hula ndege, mijusi, vyura na hata samaki.

Spishi chache za popo wanyonya-damu huko Amerika ya Kusini hula damu ya mamalia au ndege.

Familia Pteropodidae ya nusuoda Yinpterochiroptera ina spishi kubwa hadi ukubwa wa paka na uzito wa kilogramu moja; urefu wa mabawa pamoja unaweza kufikia sentimita 150. Spishi hizi hula matunda.

Remove ads

Uainishaji

Hapo awali, popo waligawanywa katika nusuoda Microchiroptera na Megachiroptera. Walakini, tafiti za ADN zilifunua kuwa baadhi ya familia za Microchiroptera zilikuwa karibu na Megachiroptera. Kwa hivyo, nusuoda mbili mpya zilipendekezwa, Yangochiroptera na Yinpterochiroptera. Nusuoda ya mwisho imegawanywa katika familia za juu Pteropodoidea (popo-matunda) na Rhinolophoidea (popo-wadudu; spishi mbalimbali hula vertebrata wadogo).

Remove ads

Utambuaji kwa mwangwi

Popo wengi hutumia sauti kwa kutambua mazingira yao, yaani wanatumia mwangwi wa mlio wao kukadiria umbali hadi kizuizi au hata windo pamoja na ukubwa na maumbile ya vitu vilivyopo njiani. Kwa hiyo masikio yao ni mlango wa fahamu muhimu zaidi. Kinyume chake popo wengi hawana macho mazima ingawa hakuna aliye kipofu kabisa. Lakini kuna pia aina nyingine wanaoona vizuri sana.

Picha

Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Popo kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads