Nguo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Nguo ni kitambaa ambacho kinaweza kutumika kufunikia meza, kitanda n.k. lakini hasa kutengenezea mavazi mbalimbali yanayovaliwa na mtu kwa ajili ya kujisitiri, kwa sababu ya kutunza heshima yake na kujikinga dhidi ya baridi, jua, mvua n.k. Ndiyo sababu mara nyingi neno "nguo" linamaanisha mavazi yenyewe.

Nguo huvaliwa kulingana na hali ya hewa na mazingira fulani, lakini pia kulingana na mitindo inayobadilikabadilika kadiri ya nyakati.
Remove ads
Historia ya nguo
Kulingana na wanaakiolojia na wanaanthropolojia, nguo za kwanza zilikuwa manyoya, ngozi za wanyama, majani na nyasi. Uvaaji wa nguo hizi uliwasaidia binadamu haswa katika kujikinga na hewa baya, kujikinga na vumbi pamoja na dhoruba kali.
Tanbihi
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads