Pafnusi wa Tebe

From Wikipedia, the free encyclopedia

Pafnusi wa Tebe
Remove ads

Pafnusi wa Tebe alikuwa mmonaki mfuasi wa Antoni Mkuu na wa Makari Mkuu, halafu askofu wa mji fulani wa Thebaid kaskazini (Misri) mwanzoni mwa karne ya 4.

Thumb
Pafnusi wa Misri (karne ya 16 au 17).

Wataalamu wengine wanamhesabu kati ya wahusika muhimu wa Mtaguso wa kwanza wa Nisea (325), alipotetea kwa nguvu zote imani sahihi, na wanasema aliongozana na Atanasi wa Aleksandria kushiriki Sinodi ya kwanza ya Turo (335).

Kabla ya hapo alidhulumiwa na serikali ya Dola la Roma akaharibiwa mguu wa kushoto na jicho la kulia kwa sababu ya imani yake akapelekwa kufanya kazi ya shokoa migodini wakati wa kaisari Galerius [1].

Tangu zamani anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 19 Aprili [2]; katika Kanisa la Kilatini tarehe 11 Septemba[3][4].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo kwa Kiswahili

Marejeo mengine

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads