Petro Nolasco

From Wikipedia, the free encyclopedia

Petro Nolasco
Remove ads

Petro Nolasco (kwa Kifaransa Pierre Nolasque; alizaliwa Mas-Saintes-Puelles, Ufaransa, 1189 hivi - Barcelona, leo nchini Hispania, 6 Mei 1256) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki anayekumbukwa hasa kwa juhudi zake za kukomboa Wakristo waliotekwa na Waislamu utumwani pamoja na kurudisha amani [1].

Thumb
Mtume Petro akimtokea Mt. Petro Nolasco; mchoro wa Francisco de Zurbarán, Museo del Prado, Madrid (Hispania.)

Kwa ajili hiyo alianzisha, pamoja na padri Raimundi wa Penyafort na mfalme Yakobo I wa Aragona, utawa wa Wamersedari naye mwenyewe mwaka 1245 huko Algiers alijitoa kutekwa kwa niaba yao akapigwa hata karibu kufa.

Alitangazwa mtakatifu na Papa Urbano VIII tarehe 30 Septemba 1628.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 6 Mei kila mwaka[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads