Prokopi Mkuu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Prokopi Mkuu
Remove ads

Prokopi Mkuu (Yerusalemu, Palestina, karne ya 3 - Kaisarea Baharini, leo nchini Israeli, 8 Julai 303) alikuwa Mkristo aliyeuawa kwa kukatwa kichwa katika mji huo mara alipoanza kutetea kwa ushujaa imani yake mahakamani mwanzoni mwa dhuluma ya kaisari Diokletian[1].

Thumb
Picha takatifu ya Mt. Prokopi.

Kabla ya hapo aliishi kwa uadilifu na wema[2], pamoja na kuwa mtaalamu wa falsafa na teolojia[3][4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 8 Julai[5] au 22 Novemba[3][4].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads