Rostam Abdulrasul Aziz
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Rostam Abdulrasul Aziz (amezaliwa 21 Agosti 1964) ni mfanyabiashara / mjasiriamali na mwanasiasa kutoka Tanzania. Aliripotiwa mnamo 2013 kuwa bilionea wa kwanza wa dolar za Marekani nchini Tanzania, akimiliki mali ya jumla ya thamani ya dolar bilioni 1. [1]
'
Remove ads
Alikuwa mbunge wa jimbo la Igunga katika Mkoa wa Tabora kuanzia mwaka 1994 hadi alipojiuzulu mwaka 2011. [2] Alikuwa mtunza hazina wa kitaifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka 2005 hadi 2007 na mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM kutoka 2006 hadi 2011.
Katika jimbo lake la uchaguzi alianzisha mradi wa bima ya afya ya jamii iliyokuwa wa kwanza katika Afrika Mashariki ambako kila kaya katika jimbo lake ilipatiwa bima ya afya kutoka Mfuko wa Afya ya Jamii. Alipanua pia mfumo wa maji hadi kila mkazi katika jimbo lake aliweza kutumia maji safi. Jimbo la Igunga liliendelea kuwa wilaya ya kwanza ya Tanzania yenye kituo cha afya katika kila kijiji na umeme katika kila kata.
Kulingana na gazeti la Forbes [3] Rostam Aziz mnamo mwaka 2016 alimiliki karibu 18% ya Vodacom Tanzania ambayo ni kampuni kubwa ya simu za rununu nchini, yenye wanachama 15,000,000. [4] Rostam aliwahi kushika asilimia 35 za hisa za Vodacom kupitia kampuni yake ya Cavalry Holdings, lakini kwenye Mei 2014 aliuza asilimia 17.2 za hisa za Vodacom Tanzania kwa Vodacom Group ya Afrika Kusini kwa bei iliyokadiriwa kuwa $ milioni 250. [5]
Anamiliki pia kampuni ya Caspian Mining inayochimba migodi na kutekeleza miradi ya ujenzi[6], pamoja na kuwa na nyumba huko Dubai na Oman.
Aziz alianza biashara katika kampuni ya familia yake akaendelea kujenga himaya yake menyewe.
Remove ads
Asili
Rostam alizaliwa katika familia ya Wabaluchi Watanzania waliofika kutoka Uajemi na kukaa nchini tangu vizazi vitano. [7] Wamekaa Tanganyika baada ya kufika awali huko Zanzibar mnamo 1850. Mwanzoni familia ilianza kama wakulima wa katani, mchele na miwa.
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads