Theobadi wa Provins

From Wikipedia, the free encyclopedia

Theobadi wa Provins
Remove ads

Theobadi wa Provins, O.S.B. Cam. (kwa Kifaransa: Thibaud; 103330 Juni 1066) alikuwa mtoto wa mtawala wa Champagne, Ufaransa[1], aliyevutiwa sana na maisha ya Yohane Mbatizaji na ya Mababu wa jangwani[2], hivyo akaenda kujiunga na monasteri huko Reims.

Thumb
Sanamu yake huko Joigny.

Baadaye, akiongozana na rafiki Walter, aliishi kama mkaapweke katika mahali na nchi mbalimbali ili kukwepa watu waliowatafuta ili kuwaheshimu[3].

Kabla hajafa alipewa upadrisho ili kuongoza vizuri zaidi wanafunzi alioanza kupokea akajiunga na Wabenedikto Wakamaldoli huko Sassano, Italia[4].

Papa Aleksanda II alimtangaza mtakatifu mwaka 1073.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 30 Juni[5].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads