Tiripsi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Tiripsi
Remove ads
Remove ads

Tiripsi au vithiripi ni wadudu wadogo sana wa oda Thysanoptera (thysanos = nyoya yabisi, ptera = mabawa) katika nusungeli Pterygota (wenye mabawa). Wanatokea kila mahali pa dunia isipokuwa Antakitiki. Wadudu hawa ni wadogo kabisa. Spishi nyingi ni mm 1 tu au ndogo zaidi na hula kuvu na spora zao (aina za vijimbegu vya kuvu) au hufyonza maji ya seli za mimea. Spishi nyingine hula wadudu wadogo wengine na zinafika zaidi ya mm 1, lakini spishi za jenasi Idolothrips, zinazokula spora za kuvu, ni kubwa kuliko zote na zinaweza kufika mm 14. Kwa sababu ya ukubwa wao mdogo tiripsi wana mabawa sahili: umbo wa mrija bila vena wenye matamvua ya manyoya. Mandibulo ya kulia imepungua mpaka kubaki kama salio tu au imetoweka kabisa. Ile ya kushoto imekuwa sindano ya kupenya tishu ya mmea au mdudu. Koromeo iingizwa ili kufyonza maji ya seli. Kwa sababu ya hii tiripsi ni wasumbufu wakiwa wengi juu ya mimea iliyopandwa shambani.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Thumb
Mchoro wa tiripsi fulani
Remove ads

Picha

Makala hii kuhusu mdudu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tiripsi kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Remove ads
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads