Tukiko

From Wikipedia, the free encyclopedia

Tukiko
Remove ads

Tukiko alikuwa Mkristo wa karne ya 1 kutoka mkoa wa Asia ambaye alimfuata Mtume Paulo katika baadhi ya safari zake, na ambaye anatajwa kwa sifa katika vitabu vitano vya Agano Jipya (Mdo 20:4; Ef 6:21-22; Kol 4:7; Tito 3:12; 2 Tim 4:12). Paulo mwenyewe anamuita "Ndugu mpendwa, mtumishi mwaminifu na mwenzi katika huduma ya Bwana"[1][2].

Thumb
Mtume Paulo akiandika barua kwa Waefeso akiwa pamoja na Tukiko.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 29 Aprili[3][4].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads