Tito

From Wikipedia, the free encyclopedia

Tito
Remove ads
Remove ads

Tito (labda 12 - 107) ni mmojawapo kati ya viongozi wa kwanzakwanza wa Kanisa, akiwa mwenzi na mwandamizi wa Mtume Paulo, anayetajwa katika Nyaraka zake mbalimbali.

Thumb
Mt. Tito askofu.
Thumb
Kanisa lake huko Heraklion.

Alikuwa naye huko Antiokia akaongozana naye kwenye Mtaguso wa Yerusalemu,[1] ingawa jina lake halitajwi katika kitabu cha Matendo ya Mitume.

Kabla hajabatizwa alikuwa Mpagani, hivyo Paulo alikataa kabisa dai la kwamba atahiriwe ili aokoke.

Kadiri ya Nyaraka, baadaye alikuwa naye Efeso, akatumwa Korintho.[2]

Walikutana tena Makedonia,[3] halafu akawa kisiwani Krete ili kuimarisha uongozi wa Kanisa la huko.[4]

Habari za mwisho ni kwamba alikwenda Dalmatia [5].

Agano Jipya halisimulii kifo chake.

Mapokeo yanasema Paulo alimpa daraja ya uaskofu kwa ajili ya Gortyn huko Krete, na kwamba alifariki mwaka 107, akiwa na umri wa miaka 95.

Tangu mwaka 1969, Kanisa Katoliki la Kilatini linamwadhimisha pamoja na Timotheo tarehe 26 Januari, siku inayofuata ile ya Uongofu wa Mt. Paulo, mwalimu wao.[6][7][8]

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading content...
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads