Wahu

Mwimbaji-mtunzi wa nyimbo , mwanamitindo wa zamani, mwigizaji na mjasiriamali kutoka Kenya From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Rosemary Wahu Kagwi, [1] anajulikana kitaaluma kwa jina moja la Wahu, ni mwimbaji na mtunzi wa nyimbo kutoka Kenya, mwanamitindo wa zamani, mwigizaji na mjasiriamali.

Maisha ya awali na elimu

Alizaliwa mwaka 1980 huko Nairobi. Wahu alisoma shule ya msingi ya Hospital Hill na kuendelea hadi shule ya upili ya Precious Blood mbayo iko Riruta . Akiwa shuleni, aliandika wimbo wake wa kwanza. [2] Wahu ni mwanamitindo wa zamani na mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Nairobi, aliyehitimu shahada ya Sanaa katika hisabati na Mawasiliano .

Kazi

Alianza kazi yake ya muziki mnamo mwaka 2000. Alitoa wimbo wake wa kwanza "Niangalie" ambao ulipata mapokezi mazuri barani Afrika na duniani kote kwa ujumla. Nyimbo zake tatu za kwanza zilikuwa "Niangalie", "Esha" na "Liar". Wahu alitoa wimbo wake mkuu wa kwanza, "Sitishiki" karibu 2005. [3] Baadhi ya muziki wake umetayarishwa na ma DJ wa Ogopa . Wahu ameburudisha hadhira pamoja na Wasanii wengi wa Kenya na Afrika kama Kleptomaniacs, Fally Ipupa, Nonini, Nameless, Wyre, Qqu, na P-Unit . Yeye ndiye mpokeaji wa kwanza wa Tuzo za Muziki za MTV Afrika 2008, [4] kwa kitengo cha Msanii Bora wa Kike. Zaidi ya hayo, ameshinda Tuzo za Pearl of Africa Music Awards, Chaguo La Teeniez na Kisima Music Awards . [5] Katika tasnia ya uigizaji, Wahu alikuwa na nafasi kubwa katika kipindi cha televisheni cha Tazama

Remove ads

Maisha binafsi

Ameolewa na David Mathenge almaarufu Nameless, mwanamuziki mwingine wa Kenya. Wana watoto wa kike 2 wanaoitwa Tumiso na Nyakio. Alijitolea wimbo wake mkubwa zaidi hadi sasa "Sweet Love" kwa mmoja wa binti zake. [3]

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads