Wapentekoste

From Wikipedia, the free encyclopedia

Wapentekoste
Remove ads

Wapentekoste ni jina linalojumuisha Wakristo wanaofuata tapo la Kipentekoste linalolenga kuleta upyaisho katika Kanisa kwa kutia maanani tukio la sikukuu ya Pentekoste ya mwaka uleule wa kifo na ufufuko wa Yesu.[1]

Thumb
"Apostolic Faith Mission" kwenye Azusa Street inahesabiwa kuwa chanzo cha tapo la Kipentekoste.
Thumb
Waumini wa Pentecostal Church of God huko Lejunior, Kentucky, Marekani wakimuombea msichana mwaka 1946.

Tapo hilo linaungana na Waprotestanti wengine katika kushikilia Biblia ya Kikristo tu na kwa njia yake kumkiri Yesu kuwa Bwana na kumpokea kama mwokozi, lakini pia linasisitiza mang'amuzi binafsi ya Roho Mtakatifu katika maisha ya muumini kama yalivyotokea mwanzoni kadiri ya Matendo ya Mitume ili kuwezeshwa kuishi Kikristo kweli kwa upako wa Roho.

Kwa kuwa wanajitangaza "wameokoka", yaani wameachana na dhambi, kwa Kiswahili wanaitwa pia "Walokole".

Tangu tapo hilo lilipoanza mwaka 1907 huko Marekani, Wapentekoste wameshakuwa zaidi ya milioni 279, mbali ya Wakristo wa madhehebu ya zamani walioathiriwa nalo ambao wanaitwa mara nyingi Wakarismatiki na ambao idadi yao inalingana na hiyo.

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads