Yosefu Maria Robles

From Wikipedia, the free encyclopedia

Yosefu Maria Robles
Remove ads

Yosefu Maria Robles (kwa Kihispania José Maria Robles Hurtado, Mascota, Jalisco, Mexico, 3 Mei 1888 - Quila, Jalisco, 26 Juni 1927) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki nchini Meksiko hadi alipouawa kwa kutundikwa mtini bila kesi wakati wa Vita vya Wakristero.

Thumb
Mt. Yosefu Maria.

Kwa miaka 14 alikuwa amehudumia kwa upendo mkubwa waamini wake, pamoja na kuandika vitabu vya Kikristo na kuanzisha shirika la Masista wa Moyo Mtakatifu wa Yesu[1].

Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwenye heri tarehe 22 Novemba 1992 halafu mtakatifu mfiadini tarehe 21 Mei 2000 pamoja na wenzake 24 waliofia dini katika vita hivyo[2]:

Sikukuu yao inaadhimishwa kila tarehe 21 Mei ila ya kwake mwenyewe ni tarehe ya kifodini chake[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads