Yosefu wa Studion

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Yosefu wa Studion (Konstantinopoli, leo nchini Uturuki, 760 hivi – Thessalia, Ugiriki, 15 Julai 832) alikuwa mmonaki kama familia yake yote, pia mtunzi wa tenzi na matini mengine ya liturujia[1], halafu askofu mkuu wa Thesalonike kuanzia mwaka 806/807 hadi alipoondolewa madarakani.

Anakumbukwa pia kwa kumlaumu kaisari na kwa kutetea kwa nguvu picha takatifu, bila kujali kwamba msimamo wake ulimvutia tena na tena dhuluma pamoja na kaka yake Theodoro wa Studion hata akafariki uhamishoni kwa njaa[2].

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 15 Julai[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads