Blandina (kwa Kifaransa: Blandine; alifariki Lyon, leo nchini Ufaransa, 177) alikuwa mwanamke mtumwa aliyeuawa katika dhuluma wa kaisari Marcus Aurelius dhidi ya Wakristo[1].

Thumb
Picha takatifu ya Mt. Blandina.
Fresque de la chapelle orthodoxe de la Dormition de la Mère de Dieu (Drôme).

Barua iliyotufikia kutoka kwa walionusurika kuuawa wakati huo inaleta ripoti kali lakini sahihi ya mauaji hayo ya wafiadini wa Lyon yaliyofanyika katika mji mkuu wa Gallia. Yeye alikuwa wa mwisho kuuawa: baada ya kuhamasisha wenzake wastahimili mateso pamoja na mwenyewe kuyapata kuliko wote, alichinjwa kwa upanga.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu bikira na mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 2 Juni[2] pamoja na ya wenzake 47: askofu Potinus wa Lyon, Aleksanda, Attalus, Vezi Espagati, Maturus, shemasi Sanctius, padri Zakaria, Makari, Asklibiade, Silvio, Primo, Ulpio, Vitale, Komino, Oktoba, Filomeno, Gemino, Julia, Albina, Grata, Emilia, Potamia, Pompea, Rodana, Biblis, Kwarsya, Materna, Elpis, Pontiko, Isto, Aristeo, Korneli, Zosimo, Tito, Julius, Zotiko, Apoloni, Jeminiani, Julia mwingine, Ausona, Emilia mwingine, Iamnika, Pompea mwingine, Domna, Yusta, Trofima na Antonia. Baadhi walifia gerezani, baadhi waliuawa katika kiwanja cha michezo mbele ya maelfu ya watazamaji, ama kwa kwa kukatwa kichwa ama kwa kutupwa waliwe na wanyamapori.

Tazama pia

Tanbihi

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.