G ni herufi ya 7 katika alfabeti ya Kilatini ambayo ni pia mwandiko wa Kiswahili cha kisasa. Asili yake ni katika alfabeti ya Kilatini.

Maelezo zaidi Alfabeti ya Kilatini (kwa matumizi ya Kiswahili) ...
Funga

Maana za G

Historia ya alama G

Alama ya G ilianzishwa katika alfabeti ya Kilatini kama badiliko la herufi C.

Maelezo zaidi Kiebrania gimel, Kifinisia gimel ...
Kiebrania
gimel
Kifinisia
gimel
Kigiriki
Gamma
Kiitalia
cha awali: C
Kilatini
C (=g / k)
ג Thumb Thumb Thumb Thumb
Funga

Asili ya herufi G ni pamoja na C katika miandiko iliyotangulia alfabeti ya Kilatini. Waroma walipokea mwandiko kutoka alfabeti ya Kigiriki kupitia alfabeti za Kiitalia za awali kama Kietruski. Wagiriki walipokea kutoka Wafinisia.

Wafinisia walikuwa na gimel iliyokuwa kiasili picha iliyorahisishwa ya ngamia wakitumia alama tu kwa sauti ya "g" na kuiita kwa neno lao kwa ngamia "gimel". Wagiriki walichukua alama hiyo na kuiita "gamma" bila kujali maana asilia ya "ngamia" ilikuwa sauti tu ya "g".

Waitalia ya kwanza hawakuwa na sauti ya "g" wakatumia alama kwa aina ya "k". Waroma wakaipokea hivyo lakini walikuwa na sauti ya "g" hivyo mwanzoni walitumia "C" kwa sauti zote mbili za "G" na "K". Baadaye waliona vema kutofautisha kati ya sauti za "k" na "g" wakaongeza mstari kwenye C kuifanya G. "C" ikabaki kwao kwa kuandika sauti ya "k".

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.