From Wikipedia, the free encyclopedia
Taiga (kwa Kiingereza[1] pia boreal forest [2] au snow forest [3]) ni jina la maeneo makubwa ya misitu kaskazini mwa dunia inayofanywa na aina mbalimbali ya miti ya misunobari, katika Eurasia pia pamoja na mibetula. Takriban 29% za misitu yote duniani ni aina ya taiga.
Taiga inafunika sehemu kubwa za Alaska, Kanada, Uswidi, Ufini, Norwei, Kazakhstan ya kaskazini na Urusi (hasa Siberia) pamoja sehemu nyingine za kaskazini za Marekani.
Maeneo ya taiga yako upande wa kusini wa kanda la tundra. Katika Urusi taiga inafuatwa na kanda la mbuga baridi kusini mwake.
Kwa jumla tabianchi kwenye taiga ni baridi sana kwa miezi mingi ya mwaka[4]. Majirajoto ni fupi, kwa kawaida miezi 1-2 pekee. Taiga ya Siberia wastani ya halijoto wakati wa baridi ni kati ya -6°C na -50°C.[5]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.