Amu Darya
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Amu Darya (kwa Kiajemi: آمودریا) ni mto mkubwa katika Asia ya Kati. Unaundwa na muungano wa mito ya Vakhsh na Panj. Katika nyakati za zamani mto huo uliangaliwa kama mpaka kati ya Iran na Asia ya Kati.

Remove ads
Majina ya kihistoria

Mazingira ya mto huu yalikaliwa kwa milenia na watu wa makabila na mataifa waliobadilikabadilika wakitunza kumbukumbu katika maandiko. Kwa hiyo kuna majina mbalimbali yaliyohifadhiwa.
Zamani za Waarya waliohamia Uhindi kutoka Asia ya Kati takriban miaka 4000 iliyopita, mto ulitwa nao "Vaksu".
Wagiriki na Waroma wa Kale waliujua kwa jina la Oxos katika Kigiriki na Oxus katika Kilatini.
Jina la kisasa lina asili ya Kiajemi: limefanywa na maneno Amu na Darya. "Amu" (Amul, leo Türkmenabad) lilikuwa jina la mji kando ya mto uliokuwa kituo muhimu kwenye barabara ya hariri. "Darya" ni neno la Kiajemi kwa mto au bahari.
Remove ads
Njia ya mto
Chanzo cha maji yake ni hasa theluji ya barafuto mbalimbali katika milima ya Pamir inayolisha matawimto yanayoingia katika Amu Darya. Mto unabeba maji yake kaskazini ambako njia yake inaingia katika maeneo yabisi na hatimaye jangwani hadi kufika kwenye beseni la Ziwa Aral. Ziwa hilo lililishwa kwa milenia na maji ya Amu Darya. Lakini miradi mikubwa ya umwagiliaji iliyoanzishwa katika karne ya 20 ilipunguza kiasi cha maji kwenye mto; Ziwa Aral lilianza kupungua hadi kupotea na zaidi ya asilimia 90 ya eneo lake. Hata mto wenyewe haufiki tena ziwani bali unaishia jangwani kabla ya ziwa.

Urefu wa mto wote ni km 2400 na beseni lake ni eneo jumla ya km2 534,739. Maji yote hutoka kwenye milima mirefu kusini ambapo hali ya hewa ya kila mwaka inaweza kuwa zaidi ya mm 1,000. Hata kabla ya kuanzishwa kwa miraddi mikubwa ya umwagiliaji, takriban asilimia 40 ya maji zilipotea jangwani kwa njia ya uvukizaji.
Remove ads
Historia

Watu walianza kujenga makazi ya kudumu kwenye karne ya 5 BK wakianza pia kulima.
Amu Darya iliitwa Oxus na Wagiriki wa zamani. Katika nyakati za zamani, mto Anu arya ulizingatiwa kama mpaka kati ya Irān na Turan (Asia ya Kati). [1]
Beseni la Am Darya lilikuwa mara nyingi kama mpaka baina ya tamaduni na milki kubwa. Kwa mfano milki ya Aleksander Mashuhuri ilipata hapa mpaka wake wa kaskazini-mashariki, na milki ya Chingis Khan ilikuwa hapa na mpaka wake wa kusini.
Barabara ya hariri kutoka China kwenda Mashariki ya Kati ilitumia bonde la Amu Darya na kuwezesha ukuaji wa miji tajiri.
Katika karne ya 19 Urusi uliingiza Asia ya Kati katika milki yake. Nafasi yake ilichukuliwa na Umoja wa Kisovyeti kwa miongo mingi ya karne ya 20. Katika mfumo wa uchumi wa kikomunisti maji ya Amu Darya yalitumiwa kubadilisha nyika yabisi za Asia ya Kati kuwa nchi ya kilimo. Miradi mikubwa ya umwagiliaji ilipeleka maji yake mbali, hasa kwa kuwezesha mashamba makubwa ya pamba. Mifereji wa Qaraqum, Karshi na Bukhara ilikuwa kati ya njia kubwa zilizojengwa za kupeleka maji ya mto hadi mashamba yale. [2] Katika itikadi ile hifadhi ya mazingira haikuwa na umuhimu sana. Mifereji haikufunikwa, hivyo kuongeza upotevu wa maji kwa njia ya uvukizaji.
Baada ya kuporomoka kwa ukomunisti beseni la Amu Darya liligawiwa kwa nchi mpya tofauti na usimamizi wa miradi haukuwa mzuri. Upotevu wa maji uliongezeka kwa sababu saruji ya mifereji iliyozeeka ilianza kuvunjika na hivyo kupotea maji zaidi.

Tanbihi
Marejeo mengine
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads