Aswan

From Wikipedia, the free encyclopedia

Aswan
Remove ads

Aswan (kwa Kiarabu أسوان, Aswān, pia Assuan au Assouan) ni mji wa kusini kabisa nchini Misri wenye wakazi 200,000. Ni makao makuu ya mkoa wa Aswan. Imejulikana duniani kutokana na lambo la Aswan ambalo ni ukuta mkubwa unaozuia mwendo wa mto Nile na kusababisha kutokea kwa bwawa la Nasser.

Ukweli wa haraka Nchi, Mkoa ...
Thumb
Msikiti mkuu wa Aswan
Thumb
Kanisa kuu la Kikopti la Aswan

Tangu kutengenezwa kwa lambo hilo, Aswan imekuwa mji wa viwanda kwa sababu umeme unapatikana kwa wingi tangu 1960.

Utalii ni muhimu pia, kwa sababu karibu na Aswan kuna mabaki mengi ya mahekalu na majengo mengine ya enzi za Misri ya Kale.

Remove ads

Historia

Zamani mji ulijulikana kwa jina la Syene au Swan au Seveneh. Inatajwa hata katika Biblia. Ilikuwa mji muhimu wa Misri ya kusini na mara nyingi mpaka na madola ya Sudan. Hivyo Mafarao waliweka huko kituo muhimu cha kijeshi kwa karne nyingi.

Aswan ilikuwa muhimu katika historia ya sayansi. Wazee walitambua ya kwamba wakati wa mchana jua liko juu kabisa angani na fimbo halina kivuli katika saa ya adhuhuri. Mtaalamu Mmisri Eratosthenes alianza hapa upimaji wake uliothibitisha ya kuwa dunia si tambarare, bali duara kama mpira.

Remove ads

Tazama pia

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu maeneo ya Misri bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Aswan kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads