Ayuki

From Wikipedia, the free encyclopedia

Ayuki
Remove ads

Ayuki (ing. na lat. Capella ka-pel-la, pia α Alpha Aurigae, kifupi Alpha Aur, α Aur) ni nyota angavu zadi katika kundinyota la Hudhi (Auriga). Ni pia nyota angavu ya sita kabisa kwenye anga. Mwangaza unaoonekana ni 0.08 mag. Iko karibu na Dunia ikiwa umbali wa miaka nuru 43.[1]

Ukweli wa haraka
Thumb
Ayuki - Capella katika kundinyota Hudhi (Auriga)
Remove ads

Jina

Ayuki ilijulikana kwa mabaharia Waswahili tangu miaka mingi wakifuata njia yao baharini wakati wa usiku kwa msaada wa nyota. [2]. Walipokea jina hili kutoka kwa Waarabu waliosema العيوق al-ayuq ambalo linamaanisha “Kizuizi” au “Kitenganishi” kwa sababu waliona nyota hii inatenganisha Dabarani na Kilimia [3].

Hapa hawakutafsiri jina la Wagiriki waliosema "Αιξ" aiks yaani mbuzi.[4]. Hapa walifuata Wababeli wa Kale waliotangulia kuona hapa mbuzi.

Katika picha ya Hudhi inayodhaniwa angani Ayuki iko mbegani wa kushoto.

Jina la Kilatini lililopokelewa na kuthibitishwa na UKIA ni “Capella” [5] na maana ya jina ni « mbuzi mdogo ».

Katika mitholojia ya Kigiriki kuna masimulizi ya mungu Zeus aliyefichwa baada ya kuzaliwa kwa sababu babake mungu Kronos alimeza watoto wake wote; hivyo Kronos alidanganywa kwa kupewa jiwe katika vitambaa vya mtoto na Zeus mdogo alifichwa kwenye kisiwa cha Krete katika pango na humo alilishwa na mbuzi.

Remove ads

Tabia

Ayuki - Capella ilitambuliwa baada ya kupatikana kwa darubini bora zaidi si nyota moja bali nyota maradufu katika mfumo wa nyota nne. Zinakaa kama jozi mbili za mapacha.

Jozi ya kwanza ni nyota mbili kubwa zinazoitwa Capella Aa na Capella Ab. Jozi ya pili ni nyota ndogo zinazokaa kwa umbali wa vizio astronomia 9,500 kutoka Aa-Ab na hizi zinaitwa Capella H na Capella L.

Aa ni nyota jitu jekundu iliyomaliza tayari akiba ya hidrojeni na sasa inayeyunganisha heli yake kuwa kaboni na oksijeni. Spektra yake ni ya aina G8III. Masi yake ni mara 2.69 masi ya Jua ikiwa na ng'aro mara 78.5 ya Jua letu. solar luminosities (Capella Aa), 77.6 (Capella Ab),.

Ab ina masi ya jua mara 2.56 na spektra yake ni ya aina G0-1 III. Aa na Ab zinazungukana kwa umbali wa kizio astronomia 0.72 au kilomita milioni 108 katika muda wa siku 104.

Nyota za H (aina ya spektra M1-M2.5) na L (spektral M5) ni nyota kibete nyekundu inayozungukana kwa umbali wa vizio astronomia 49

Remove ads

Tanbihi

Viungo vya Nje

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads