Bethsaida

From Wikipedia, the free encyclopedia

Bethsaidamap
Remove ads

Bethsaida (kutoka Kiebrania/Kiaramu בית צידה beth-tsaida, yaani "Nyumba ya uwindaji" au "ya uvuvi", kutoka mzizi צדה auצוד)[1] ni mahali panapotajwa na Agano Jipya.

Thumb
Bethsaida

Palikuwa upande wa mashariki wa mto Yordani, labda jirani na mahali ambapo mto huo unaingia katika Ziwa Galilaya. [2]

Bethsaida ndio mji asili wa mitume wa Yesu wafuatao: Petro, Andrea nduguye na Filipo (Yoh 1:44).

Bethsaida inatajwa na Mk 8:22-26 kama mji (κώμη) ambapo Yesu alimponya kwa awamu mbili mwanamume kipofu.

Ingawa katika Injili hakuna habari za miujiza mingine iliyofanyika huko, Yesu aliutishia mji huo laana ya milele kwa kutopokea ujumbe wake wa toba.

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads