Jerboa

ukarasa wa maana wa Wikimedia From Wikipedia, the free encyclopedia

Jerboa
Remove ads

Jerboa ni wanyama wagugunaji wa nusufamilia Allactaginae, Cardiocraniinae, Dipodinae na Euchoreutinae katika familia Dipodidae wanaofanana na kanguruu wadogo kwa sababu wana miguu mirefu ya nyuma na miguu mifupi ya mbele. Wanatokea maeneo makavu katika Afrika ya Kaskazini na Asia.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Remove ads

Maelezo

Jerboa ni wagugunaji wadogo hadi wa kadiri wenye urefu wa mwili wa sm 4-26 bila mkia, ambao ni mpaka maradufu wa urefu wa mwili. Wote wametoholewa kwa kuruka ingawa kwa viwango tofauti. Wana miguu mirefu sana ya nyuma ambayo, katika spishi nyingi, inajumuisha mifupa mirefu ya metakarpali. Wanasonga ama kwa kuruka au kwa kutembea kwa miguu yao ya nyuma. Mkia mrefu wa jerboa husaidia katika kuweka usawaziko wao.

Wengi ni walavyote na lishe yao ni mbegu na wadudu. Spishi kadhaa za jerboa hata hivyo, kama Allactaga sibirica, ni karibu walawadudu kabisa. Kama wagugunaji wengine wana meno ya mbele ya kutafuna yaliyotengwa kwa pengo (diastema) na meno ya shavu ya kusaga.

Jerboa hufanya viota vyao kwenye vishimo ambavyo vinaweza kuwa tata kwa vyumba vya pembeni ambapo huhifadhi chakula chao. Spishi nyingi hulala wakati wa baridi kwa angalau nusu mwaka zikinusurika kwa mafuta zinayounda katika wiki kadhaa kabla ya kulala.

Majike huzaa wachanga wawili hadi saba baada ya kipindi cha ujauzito kati ya siku 17 na 42. Wanazaana mara moja au mbili kwa mwaka kulingana na spishi.

Remove ads

Spishi za Afrika

Spishi za Asia

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads